Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (katikati) na Mwenyekiti wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro, Bi. Asia Ashirafu (wa pili kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Klabu hiyo na viongozi wa THBUB wanafunzi hao walipotembelea Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma leo Januari 26, 2024. Wa kwanza kulia (waliokaa) ni Kiongozi wa msafara wa Klabu hiyo, Bwana Yusuf Said.
Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Mathew Mwaimu (Jaji Mst.), akiongea na wanachama wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro (hawapo pichani) leo Januari 26, 2024, wanachama hao na walimu wao walipotembelea Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Mohamed Khamis Hamad.
Baadhi ya wanachama wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro wakipokea nasaha kutoka kwa Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Mathew Mwaimu (Jaji Mst.), leo Januari 26, 2024 Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria, THBUB, Bwana Nabor Assey akiwaeleza wanachama wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro utekelezaji wa majukumu ya Tume kupitia Idara anayoiongoza, wanachama hao walipotembelea Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma leo Januari 26, 2024.
Mkurugenzi wa malalamiko na uchunguzi, THBUB, Bi. Suzana Paschal akiwaeleza wanachama wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro utekelezaji wa majukumu ya Tume kupitia Idara anayoiongoza, wanachama hao walipotembelea Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma leo Januari 26, 2024
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (katikati) na Mwenyekiti wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro, Bi. Asia Ashirafu (wa pili kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa Klabu hiyo na viongozi wa THBUB wanafunzi hao walipotembelea Makao Makuu ya Tume, Kilimani jijini Dodoma leo Januari 26, 2024. Wa kwanza kulia (waliokaa) ni Kiongozi wa msafara wa Klabu hiyo, Bwana Yusuf Said.
Wanafunzi 70 wanachama wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro wakiambatana na walimu wanne (4) leo Januari 26, 2024 wametembelea Makao Makuu ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Kilimani jijini Dodoma na kujifunza masuala mbalimbali.
Wanafunzi hao wameipongeza Tume kwa juhudi zake za kulinda na kueneza elimu ya haki za binadamu na utawala bora nchini.
“Tumetembelea Tume na kujifunza masuala mbalimbali ya utekelezaji wa majukumu ya Tume, tumefurahi sana, hakika mnafanya kazi nzuri iliyotukuka,” amesema mmoja wa wanafunzi hao.
“Nimefurahi pia kuwaona Mheshimiwa Mwenyekiti wa Tume na Makamishna wake, na jinsi tulivyopokelewa vizuri na kwa upendo mkubwa,” ameongeza.
Wakiwa katika ofisi hizo za Tume wanafunzi hao walipata fursa ya kuwasikiliza wakurugenzi na wakuu wa vitengo vilivyopo Tume wakielezea utekelezaji wa majukumu ya taasisi hiyo kupitia idara na vitengo wanavyosimamia. Vilevile, walipata nasaha kutoka kwa viongozi wa juu wa Tume.
Wanafunzi hao wametembelea THBUB kama taasisi ya kitaifa ya haki za binadamu na mlezi wa Klabu za haki za binadamu katika taasisi za elimu nchini, ili kujifunza namna Tume inavyotekeleza majukumu yake.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Klabu ya haki za binadamu Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro, Bi. Asia Ashirafu kila mwaka Klabu hiyo imekuwa na utaratibu wa kutembelea taasisi mbalimbali za umma kwa lengo la kujifunza kama sehemu ya masomo yao.
No comments:
Post a Comment